Spika wa Baraza la Wawakilishi apokea Vitabu vya Ripoti ya CAG ya mwaka 2021/2022

Posted on: 12.05.2023

Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir ali Maulid amepokea vitabu vya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2021/2022 na kusema kuwa ripoti hizo zitaanza kufanyiwa kazi haraka ili ziweze kutoa mapendekezo  yanayohitajika.

 

Mhe Zuberi akipokea vitabu saba vya Ripoti hizo kutoka kwa Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba, Sheria na Utawala bora Mhe. Haroun Ali Suleiman amesema Ripoti hizo zitakabidhiwa katika kamati za Baraza la Wawakilishi zinazohusika na masuala ya uchunguzi wa hesabu za Serikali ili ziweze kufanyiwa kazi na baadae kuweza kutolewa ufafanuzi wa yale yaliyofichuliwa ndani ya ripoti hizo.

 

Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba, Sheria na Utawala bora Mhe Haroun Ali Suleiman amesema Ripoti alizowasilisha ni pamoja na taarifa ya Serikali kuu, Idara maalum za SMZ, Mifumo ya Tehama ya SMZ, Mashirika ya umma, Miradi ya maendeleo, Ukaguzi wa kiufundi na mfuko wa maendeleo ya jimbo na miradi ya maendeleo ya wadi.

 

Waziri Nchi Afisi ya Makamo wa Pili wa Rais, sera uratibu na Baraza la Wawakilishi Mhe Hamza Hassan Juma na Makamo Wenyeviti wa Kamati ya PAC na LAAC wamesema wataendelea kuzifanyia kazi Ripoti hizo kwa umuhimu wake ili ziweze kuchukuliwa hatua kwa pale patakapohitajika.

 

Mwisho

//