Kuanza Kazi Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi

Posted on: 30.10.2023

Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi zimeanza Vikao vyake leo tarehe 30 Oktoba 2023, ikiwa ni mzunguko wa Pili wa kazi za kawaida za Kamati. Vikao hivyo vimeanza Kisiwani Pemba na vinatarajiwa kuhitimishwa Unguja tarehe 17 Novemba, 2023.

Kamati zinafanya Vikao hivyo kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa Kumi na Tatu wa Baraza la Kumi la Wawakilishi unaotarajiwa kuanza tarehe 29 Novemba, 2023.

Kamati zilizoanza kazi leo ni Kamati ya kuchunguza na kudhibiti Hesabu za Serikali na Mashirika (PAC), Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa na  Kamati ya Bajeti

//